Menu

Zaburi 70

BIB

1 Ee Mungu, ufanye haraka kuniokoa; Ee Bwana, njoo hima unisaidie. 2 Wale wanaotafuta kuuondoa uhai wangu, waaibishwe na kufadhaishwa; wote wanaotamani kuangamizwa kwangu, warudishwe nyuma kwa aibu. 3 Wale waniambiao, “Aha! Aha!” warudi nyuma kwa sababu ya aibu yao. 4 Lakini wote wakutafutao washangilie na kukufurahia, wale wapendao wokovu wako siku zote waseme, “Mungu na atukuzwe!" 5 Lakini bado mimi ni maskini na mhitaji; Ee Mungu, unijie haraka. Wewe ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu; Ee Bwana, usikawie.

Everything we make is available for free because of a generous community of supporters.

Donate