Menu

Zaburi 133

ULB

1 Tazama, jinsi ilivyo vema na yakupendeza ndugu waishi pamoja, kwa umoja! 2 Ni kama mafuta mazuri kichwani yashukayo ndevuni. Ndevu za Haruni, na yashukayo mpaka upindo wa mavazi yake. 3 Ni kama umande wa Hermoni uangukao milimani pa Sayuni. Maana huko ndiko Bwana alipoamuru baraka, naam uzima milele na milele.

Everything we make is available for free because of a generous community of supporters.

Donate